0

Zaidi ya makokoro 90 yenye thamani ya Shilingi Milioni 56.4 yaliyokamatwa yakitumiwa na wavuvi haramu katika Ziwa MANYARA na BURUNGE Mkoani MANYARA yameteketezwa kwa moto na wahusika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Mkuu wa Mkoa wa MANYARA, JOEL BENDERA ameagiza watu watakaokamatwa na nyezo haramu za kuvulia samaki ama samaki waliovuliwa kinyume cha sheria mali zao yakiwemo magari na pikipiki zitaifishwe.

Awali katika maelezo yao Mkuu wa Wilaya ya BABATI Mhandisi RAYMOND MUSHI na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, HAMIS MALINGA wamesema uvuvi unaofanyika katika maziwa hayo si endelevu.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top