0
ZAIDI ya Wanafunzi elfu kumi wa shule za msingi mkoani MANYARA walionza Darasa la kwanza mwaka 2010 hawajamaliza shule kutokana na sababu mbali mbali zikiwemo za utoro, mimba, magonjwa na vifo.
Kaimu Afisa Elimu wa mkoa wa MANYARA LAGO SILLO amesema  idadi hiyo ni sawa na asilimia 28.33 ya Wanafunzi 36,611 walioandikishwa darasa la kwanza mwaka 2010, ambapo kati yao wanafunzi  26,239 ndio waliosajiliwa kufanya mtihani wa kumaliza Darasa la saba mwaka huu sawa na asilimia 71.67.

Katika taarifa yake wakati wa mkutano wa kuchagua Wanafunzi wa kujiunga na kitato cha kwanza mwaka ujao, Kaimu Afisa Elimu wa mkoa wa MANYARA ,LAGO SILLO amesema mkoa unahitaji nguvu ya pamoja ya kupunguza mdondoko wa Wanafunzi shuleni.

SILLO mkoa wa MANYARA umeshuka kutoka nafasi ya 19 kitaifa mwaka jana katika matokeo ya darasa la saba na kuwa mkoa wa 20 mwaka huu, licha kuwa ufaulu umeongezeka kutoa asilimia 59.18 mwaka jana hadi kufikia asilimia 62.60 mwaka huu.


Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top