0
Wenger apoteza kwa mara ya nne Ujerumani baada ya Arsenal kufungwa 1-0 na KolnBaada ya kuonyesha mchezo mzuri na kuilazaTottenham Hotspurs , mkufunzi wa Arsenal alishindwa kuilaza Koln nchini Ujerumani.
Arsenal hatahivyo watasonga katika raundi ya pili ya muondoano wakiwa viongozi wa Kundi H katika michuano ya ligi ya Yuropa, lakini hilo halikutajarajiwa kwani liliwapatia Koln matumaini ya kujiunga nao katika raundi hiyo ya pili.
Penalti ya kipindi cha pili cha mechi iliopigwa na Sehrou Guirassy iliwashangaza Arsenal na kuthibitisha kuwa Wenger hana bahati katuka mchanga wa Ujerumani.
Wenger sasa amecheza nhini Ujerumani mara nne bila kushinda.
Danny Welbeck alicheza dakika 45 katika mechi yake ya kwanza tangu mechi dhidi ya Watford wakati timu yake ilipopoteza 2-1 mnamo mwezi Oktoba na alionekana kwamba alikuwa na uwezo mkubwa wa kufunga lakini laishindwa kucheka na wavu.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top