0
Mkali wa Bongofleva Tanzania Coyo ameendelea kufanya vizuri katika kiwanda cha muziki wa kisasa Tanzania akiudhihishia Umma wa watanzania kuwa amekuja kwa ajili ya kufanya mziki kazi kwa kutoa jiwe baada ya jiwe.

Coyo amesema ngoma ambayo imemtambulisha vizuri katika sanaa ya muziki ni Njoo Baadae ambayo ataipa heshima kubwa mpaka kesho ikiwa imetengenezwa na Mr.T.Touch.

Coyo ameimbia Manyara Fm kuwa yeye mziki anafanya Popote na hategemei Dar es salaam pekee kama ilivyozoeleka kwa wengi,huku akiwapa moyo wasanii wachanga wafanye mziki mzuri unaoendana na soko la sasa.

Kwa sasa Coyo anatamba na wimbo wake mpya unajulikana kama Nyaka nyaka.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top