0
Katika kuiunga mkono serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dk. John Pombe Magufuli mkoa wa Manyara umeendelea kuwa na viwanda vidogo vidogo vinavyotoa ajira kwa vijana.
 Vilevile Mapunda amewataka vijana kuwa wabunifu ili kuweza kukabiliana na changamoto ya ajira iliyopo hapa nchini
Akizungumza na walter habari   Meneja wa  Shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo [SIDO]   iliyopo Mtaa wa nyungu Wilayan Babati Mkoan Manyara Abeli Mapunda amesema wanahudumia viwanda 2600
Mbali na viwanda kazi nyingine zinazofanywa na SIDO ni kutoa mikopo katika vikundi mbalimbali vinavyojihusisha na ujasiria mali
Hata hivyo Shirika hili lipo chini ya wizara ya Viwanda,biashara na uwekezaji ikiwa imeanzishwa na sheria ya bunge ya mwaka 1973.
Ikumbukwe kuwa sera ya serikali ya awamu ya tano ni Tanzania ya Viwanda chini ya waziri mwenye Dhamana ya viwanda Charles Mwijage ambaye amekuwa akiweka juhudi katika kuhakikisha adhima hiyo ina fanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kujenga uchumi imara wa Taifa kwa sababu hakuna nchi iliyo endelea kote ulimwenguni pasipokuwa na viwanda vya kutosha.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top