0

Image result for mji wa babatiWatu wasiojulikana wameovamia Maeneo ya katani na kufanya kilimo mpaka kuwafikia mazao kufikia hatua ya kukomaa bila kujulikana na mamlaka husika.
Madiwani wa Halmashauri ya mji wa Babati wamekutana Leo april 24.2018 katika kikao chao kuwasilisha taarifa mbalimbali za maendeleo katika kata zao ambapo mjadala mkubwa ilikuwa ni Uvamizi wa maeneo ya Maisaka katani.
Diwani wa kata ya Maisaka Abrahamani Kololi amesimama na kuomba busara itumike kwa kuwa kilichopo shambani ni chakula na sio bangi.
Hata hivyo mwanasheria wa Halmashauri ya mji wa Babati akitolea ufafunuzi wa kisheria kuhusu jambo hilo alieleza kuwa limeshakuwa la kisheria hivyo wasubiri maamuzi yatakayotolewa kwamba yateketezwe au nini kifanyike.
Mpaka sasa mazao yaliyopandwa katika maeneo hayo yanakaribia kukomaa hali inayowapa wengi maswali iliwezekanaje watu kufanya kilimo,kupanda hadi kufanya palizi bila kuonekana.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top