0
Na John Walter
Babati-Manyara
Wakati dunia imetoka kuazimisha siku ya kina Mama duniani May 14 ikifuatiwa na siku ya Familia May 15 bado vitendo vya kina Mama kunyanyasika na Familia kuvunjika vinaonekana katika jamii nyingi hapa nchini.
Siku ya Familia mwandishi wa Habari John Walter anaefanya kipindi cha mtaa kwa mtaa 92.1 Redio Manyara fm alitembelea baadhi ya Familia ili kujua namna wanavyosheherekea siku hiyo na kukutana na Mwanamama mmoja aliesimulia magumu yanaisibu Familia yake.
Katika mitaa niliyotembelea ni apmoja na Gendi uliopo mjini Babati mkoa wa Manyara ambapo alichokikuta ni tofauti alivyotarajia katika moja ya Familia huko Gendi.
Wengi wamezoea kusikia Mama akitoroka nyumbani na watoto na kuacha Nyumba lakini hii imekuwa tofauti kidogo kwenye Familia ya Sebastian Blass na Bi Magdalena Joseph ambapo Baba ndie aliechukua uamuzi wa kutoroka na watoto wake wawili aliewazaa yeye pamoja na bi Magdalena.
Bi Magdalena anasema kuwa akiwa na mwanaume huyo wamefanikiwa kupata watoto wane ambao wawili walipoteza Maisha na kubakiwa na wawili mmoja wa kiume na mwingine wa Kike ambao wote mwanaume ameondoka nao na kwenda kusikojulikana.
Akielezea kisa hicho mwanamke huyo amesema awali walikuwa wakiishi kwa upendo na amani lakini mara baada ya mwanaume huyo kutoka safarini ndipo akaanza kumfanyia visa mbalimbali huku akimwambia kuwa hamtaki aondoke na awaache watoto.
Hatua aliyoichukua mwanamke huyo alifika katika ofisi za mtaa ambapo alipatiwa barua iliyomwelekeza kwenda kituo cha polisi.
Baada ya kufika kituo cha Polisi Dawati la jinsia na watoto mjini Babati alipatiwa barua nyingine ya wito ikimtaka mwanaume kuripoti katika kituo cha polisi lakini hakufanikiwa kumpata mwanaume huyo kwani tayarai alishaondoka.
Mkaguzi msaidizi wa jeshi la Polisi kutoka dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Manyara Afande Pili Pilo alipozungumza na kipindi hiki kwa njia ya simu alionyesha kusikitishwa na kitendo hicho akielekeza kuwa mwanamke huyo atoe ushirikiano ili mwanaume huyo asakwe popote alipo na kufanyiwa mahojiano.
Nao majirani wameeleza kuwa wameshangazwa na kitendo cha mwanaume huyo kumtelekeza mwanamke wake na kwamba amemdhalilisha mwanamke wake pamoja na wanaume kwa ujumla kwa kitendo hicho ambacho sio cha kibinadamu.
Wengine wameeleza kuwa hiki ndio chanzo cha kuwepo kwa watoto wa mitaani ambao baadae yanazaliwa makundi mbalimbali ya wahalifu.

Mkoa wa Manyara ni moja kati amikoa yenye vitendo vini vya ukatili kwa wanawake na watoto haswa ukeketaji.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top